Jarida la Mapishi

Mchuzi wa viazi wenye korosho na mpopi

  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 30
  • Walaji
    4

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua mashine ya kusaga (blender). Weka kwenye hiyo mashine ya kusaga, tangawizi, vitunguu swaumu, korosho, mbegu za mpopi, pamoja na vijiko 2 vya chakula vya maji, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo umesagika vizuri na kuwa laini.

    Step2

    Weka garam masala, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo wote umechanganyika vizuri. Ondoa mchanganyiko huo kwenye mashine ya kusaga na uweke pembeni kwenye kontena.

    Step3

    Chukua sufuria kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hilo sufuria, binzari nyembamba, viazi mviringo, binzari ya manjano, pamoja na chumvi, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5 mpaka 7, au hadi utakapo ona viazi vimebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step4

    Weka mchanganyiko wa tangawizi ulio usaga kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 8 mpaka 10.

    Step5

    Mimina mtindi taratibu huku ukikoroga.

    Step6

    Mimina maji halafu koroga vizuri, kisha funika sufuria na uache ichemke kwa muda wa dakika 10, au hadi utakapo ona viazi vimeiva na mchuzi umekuwa mzito.

    Step7

    Mimina tui la nazi halafu koroga vizuri, kisha acha ichemke kwa muda wa dakika 3.

    Step8

    Weka iliki halafu koroga vizuri, kisha epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Conclusion

    Kabla ya kutumia mtindi huo, hakikisha unaupiga piga vizuri ukiwa kwenye bakuli kwa kutumia kijiko kama unavyo yapiga piga mayai unapotaka kuyakaanga, hadi utakapo ona mtindi umekuwa laini na hauna mabonge mabonge.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.